Klabu ya Simba imetangaza kuanza kwa mchakato wa kumpata mchezaji
bora wa mwezi January kwa klabu hiyo, mchakato ambao utawahusisha
mashabiki wa klabu hiyo ambao watakuwa wakipendekeza majina ya wachezaji
hao kupitia ukurasa wa Facebook wa klabu hiyo (Inbox).
Kwa mwezi Januari klabu ya SImba imecheza jumla ya michezo saba
ambapo miwili kati ya hiyo ni kwenye ligi kuu ya VPL na Mitano kwenye
kombe la Mapinduzi.
Katika michezo hiyo ya ligi kuu Simba ilicheza dhidi ya Mtibwa Sugar
January 18 ambapo iliambulia sare ya 0-0 kwenye uwanja wa Jamhuri kabla
ya kufungwa bao 1-0 na Azam FC January 28.
Katika Michuano ya Kombe la Mapinduzi Simba ilicheza dhidi ya KVC na
kuibuka na ushindi wa bao 1-0, wakatoka ya sare ya bila kufungana,
wakamfunga Jang’ombe mabao 2-0 kabla ya kumfunga Yanga kwa mikwaju ya
panati 4-2 huku wakipoteza mchezo wa fainali dhidi ya Azam kwa bao 1-0.
Kwa mwezi wa Desemba, Method Mwanjali ndie alikuwa mchezaji bora wa klabu hiyo.
0 comments:
Post a Comment