Klabu ya Simba imetangaza kuanza kwa mchakato wa kumpata mchezaji
bora wa mwezi January kwa klabu hiyo, mchakato ambao utawahusisha
mashabiki wa klabu hiyo ambao watakuwa wakipendekeza majina ya wachezaji
hao kupitia ukurasa wa Facebook wa klabu hiyo (Inbox).
Kwa mwezi Januari klabu ya SImba imecheza jumla ya michezo saba
ambapo miwili kati ya hiyo ni kwenye ligi kuu ya VPL na Mitano kwenye
kombe la Mapinduzi.