Mabingwa wa soka Tanzania bara Young Africans wameshindwa kuendelea
kuonyesha ubabe baada ya kupata ushindi finyu katika mechi yao ya Ligi ya mabigwa Afrika dhidi ya St. Louis.
Young Africans ambayo ilikuwa ikipewa nafasi ya kufanya vyema katika
michuano hiyo kwa kufika fainali na ikiwezekana kitwaa ubingwa, imeishia
hatua ya nusu fainali baada ya kufungwa kwenye Uwanja wa Amaan kisiwani
unguja dhidi ya wapinzani wao, ambao pia waliiondoa Simba katika hatua
ya makundi.
Hadi dakika za kawaida za mchezo zinakamilika matokeo yalikuwa suluhu ndipo mchezo huo uamuliwe kwa kupigwa mikwaju ya penati.
Ikiwa ndiyo siku ya
kwanza anaichezea Yanga katika michuano ya Kombe la Mapinduzi,
mshambuliaji Obrey Chirwa amekosa penati ya mwisho na kuing’oa Yanga
katika michuano ya Mapinduzi.
Chirwa alikuwa amegoma kujiunga na Yanga akitaka alipwe fedha zake za usajili. Lakini leo ameungana na kikosi hicho akitokea Dar es Salaam. Ikiwa ndiyo siku ya kwanza amejiunga na Yanga, Chirwa alitokea benchi kuchukua nafasi ya Pius Buswita na dakika 90 zikaisha kwa sare ya bila mabao, ikaingia mikwaju ya penalti.
Chirwa ndiye alikuwa wa mwisho upande wa Yanga baada ya Papy Tshishimbi, Hassan Kessy, Raphael Daud na Gadiel Michael kupata.
0 comments:
Post a Comment